MANENO YANGU NI MIMI…MANENO YANGU
NDIO MTAZAMO WANGU…MANENO YANGU
NDIO KIPIMO CHA KIASI CHA UBORA
WANGU…MANENO YANGU NDO YANAAMUA
UMBALI GANI NITAKWENDA KATIKA MAISHA NA
MAFANIKIO…
Laiti ungejua kwamba IMANI haifanyi kazi bila
MATENDO…Na matendo yanadhihirishwa na
MANENO YAKO yaliyo sawa na kile NENO LA
MUNGU limekuhakikishia…Unaanza kuwa
TAJIRI kabla ya kuwa na PESA MKONONI au
DHAHABU MGODINI…Unaanza kuwa na NDOA
njema ya KUIGWA na wote na FAMILIA yenye
KUMCHA MUNGU hata kabla hujawa na
MCHUMBA…Unaanza kuwa BABA wa MATAIFA
MENGI hata kabla ya UTAJIRI WA MATAIFA
haujakuwasilia…Unaanza KUNG’AA GIZANI na
kuwa MAJIBU YA WENGI hata kabla hujawa na
HUDUMA KUBWA machoni pa watu!
KAMA UMEFIKIA HATUA YA MANENO YAKO
YANAYOKUTOKA KWENYE KILA HALI NA
MAZINGIRA YANAOANA NA NENO LA MUNGU
[si kwa kujilazimisha, bali NENO limejaa
pomoni mpaka linamwagika] UJUE YA KUWA
UMESHAFANIKIWA…NI LAZIMA
UTAUSHANGAZA ULIMWENGU…UTAFANYA
MAMBO MAKUU…UTAKUWA JUU TU WALA SI
CHINI KAMWE!
Ila kama hujafikia hatua ya MANENO YA
MUNGU kutiririka ndani yako kwenye kila
mazungumzo yako kama mvua…Ujue bado
sana, uko mbali sana na uwanja wa
waliofanikiwa…SIKU NIKIWA MHITAJI, AU
MASIKINI, AU MGONJWA, AU KUPUNGUKIWA
NA UTUKUFU WA MUNGU, NIKISHINDWA
KUTOA MAJIBU KWA SHIDA ZANGU NA ZA
WENGINE nakupa ruhusa umtukane YESU
WANGU NA ROHO WAKE MTAKATIFU ALIYE HAI
NDANI YANGU!
MANENO YANGU YANADHIHIRISHA MIMI NI
MTU WA AINA GANI, NIMEFANIKIWA AU
NIMEKWAMA…KILA NINACHOANDIKA HAPA NI
MFUMO WANGU WA MAISHA…KWANGU
HAKUNA SURA YA MADHABAHUNI NA YA
MTAANI…KOKOTE UTAKAKOKUTANA NA MIMI
NIMEJAA MAUSIA YA MUNGU…Mimi ni
muungu, mwana wa aliye juu (Zaburi
82:6)…Nina vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa
tele(Wafilipi 4:17)…Sijawahi kukosa furaha,
amani wala matumaini…kwangu kila siku ni
sikukuu…Sina haraka, kila siku inayopita
naweka rekodi ya ushindi…sina muda wa
kusumbuka na shetani wala changamoto,
maana hazinisogelei kabisa mimi…na hata
kama zikija, nakuwa na majibu yake hata kabla
hazijabisha hodi…Ni raha sana kuwa hai hapa
duniani nikimwak