Mmiliki wa blog:

 

‘Dickson Cornel Kabigumila ni mwalimu wa Neno la Mungu. Amekuwa akifundisha katika mashule, vyuo, makanisa na fellowship za Kikristo. Amekuwa akifundisha katika ibada, semina na makongamano mbalimbali ya kiroho kwa takribani miaka 5 sasa. Alimpokea Yesu kama Bwana na mwokozi binafsi wa maisha yake mwaka 2003 na kujazwa na kubatizwa kwa Roho Mtakatifu na kwa nguvu sawa na isemavyo Matendo ya Mitume 10:38. Na amefanya kazi na mashirika na huduma mbalimbali za Kikristo kama vile TAFES, CASFETA, HUIMA, UKWATA na CHARISMATIC. Pamoja na huduma mbalimbali zinazoujenga mwili wa Kristo hapa Tanzania kama vile, MANA iliyo chini ya Mwl. Christopher Mwakasege, ambaye Mwl. Dickson hasiti kukiri kwamba amekuwa baba kwake na kwa kanisa la Tanzania, pia amefanya kazi na The Life Ministry, New Life in Christ na huduma ya kuwafikia wasiofikiwa kwa injili ya GKB. Na amewahi kuwa kiongozi wa Fellowship ya wanafunzi Wakristo wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, katika nafasi ya Mratibu wa maombi na pia kama Mwenyekiti. Na kwa neema ya Mungu, yeye ndiye mwanzilishi wa kipindi cha Mafundisho na uchambuzi wa Biblia katika siku za Jumatatu na Jumatano. Amezaliwa mwaka 1989, katika kijiji cha Chabuhora, kata ya Nyakakika, tarafa ya Nyabiyonza, Wilaya ya Karagwe, mkoa wa Kagera. Ni mtoto wa sita katika familia ya ndugu nane. Akiwa na dada zake watano na kaka wawili. Kwa kifupi huyu ndiye Mwl. Dickson Cornel Kabigumila…KARIBU.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *